Ushirika katika kuboresha mifumo kwenye Upatikanaji na Usambazaji wa Mbegu
Ushirika katika kuboresha mifumo kwenye Upatikanaji na Usambazaji wa Mbegu
Kupitia majadiliano yanayoendelea kati ya TFC na ASA, kusaini hati ya makubaliano ya kimkakati; nafasi ya vyama vya ushirika kwenye mnyororo wa mbegu na pembejeo inaendelea kupanuka.
Ushirika sasa unaweza kuwa zaidi ya mnunuzi au mpokeaji wa huduma, Vyama vinaendelea kutumia na kuboresha mifumo yenye tija huku vikiendelea kuwa;
1. Wakusanyaji wa mahitaji ya wanachama na wakulima
2. Kiunganishi muhimu kwa Wasambazaji wa mbegu na pembejeo
3. Wamiliki na Waendeshaji wa maduka na vituo vya huduma za Ugani ikwemo pembejeo
4. Wazalishaji au washiriki kwenye uzalishaji wa mbegu
5. Waunganishaji wa wakulima na fedha, bima na masoko
6. Watumiaji wa mifumo ya kidijitali ya usimamizi wa biashara ikiwemo teknolojia zinazoibukia ikiwemo Akili unde.
Kikao kazi kati ya Shirikisho la Vyama Vya Ushirika Tanzania -TFC na na wakala wa Mbegu Tanzania - ASA kilichofanyika Dar es Salaam kimeendelea kuweka msingi wa mfumo unaolenga kuhakikisha mbegu bora zinapatikana kwa wakati, kwa mpangilio bora na kupitia vyama vilivyo tayari kufanya biashara kwa weledi.
Huu ni mwendelezo na muitikio kwa vyama vya ushirika kujipanga.
1. Je, chama chako kina taarifa sahihi za mahitaji ya wanachama?
2. Je, mna uwezo wa kuhifadhi, kusambaza au kusimamia kituo cha pembejeo?
3. Je, mko tayari kuunganishwa na fedha, bima, masoko na mifumo ya kidijitali?
TFC inaendelea kuratibu taarifa na ushiriki wa wadau.
Kwa mawasiliano:
pembejeo@ushirika.co.tz
pembejeoinputs@ushirika.co.tz
CC: shirikishoushirika@gmail.com
🚀 Jiunge na Channel yetu ya WhatsApp Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (Tanzania Federation for Cooperatives - TFC) na upate taarifa zote muhimu za sekta ya ushirika zilizothibitishwa moja kwa moja kwenye simu yako.
https://whatsapp.com/channel/0029VbC4UpuDp2Q4ZMejhD3K